Wednesday, November 13, 2013

WANAWAKE UINGEREZA WALIPWA POUNDI 200 ILI WANYONYESHE WATOTO WAO

WANAWAKE wanaojifungua nchini Uingereza walipwa hadi poundi 200( Sawa na Sh.512,934 za kitanzania) ili kunyonyesha watoto wao.

Mradi huo mpya  ulioanzishwa nchini humo kwa ushirikiano kati ya serikali na watafiti wa utabibu katika mitaa ya Yorkshire Kusini na Derbyshire ili kuwahamasisha wamama kunyoshesha vichanga vyao.

Kwa mujib wa Sky New mradi huo utawafaidisha wakinamama zaidi ya 130 watakaojifungua watoto kati ya mwezi huu hadi mwkani mwezi wa tatu.

YVONNE NELSON'S BIRTHDAY BEACH PARTY WITH VAN VICKER, MAJID MICHAEL.

Ghananian star actress Yvonne Nelson celebrated her 28 birthday Yesterday 12 November in Ghana with family members, close friends and fellow actors like Van Vicker, Majid Michael, Benson Okwonko and more. It was a beach party with Yvonne flaunting her hot bikini body. Take a look............

Waigizaji wa Ghana kutoka kushoto Van Vicker akiwa na Yvonne kati pamoja na Majid Michael

                                   Wakiwa pamoja na marafiki wengine/

                                              Yvonne na Majid katika pozi

                                              Yvonne na Van Vivker


Saturday, November 9, 2013

MASHAUZI KUONGOZA UZINDULIZI WA MALAIKA HIVI KARIBUNI.

BENDI ya muziki wa taarabu ya Mshauzi Classic, Cassim Mganga na Dully Sykes, watasindikiza uzinduzi wa bendi mpya ya Malaika utakaofanyika Novemba 15, mwaka huu katika ukumbi wa Mzalendo Pub, Kijitonyama, Dar es Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa bendi hiyo, Michael Rocky, alisema tayari walikubaliana na bendi na wasanii hao kushiriki katika uzinduzi wao.

"Tuliwaomba kama wasanii wenzetu, walikubali na kutuahidi kutoa burudani nzuri katika onesho hilo maalumu la kuzaliwa kwa bendi mpya," alisema.

Alisema wasanii hao, ni miongoni mwa wasanii wanaopendwa na mashabiki wa muziki kutokana na tungo zao kuwa na ujumbe mzuri.

Rocky ambaye aliwahi kuiongoza Akudo Impact kwa mafanikio, alisema watatumia uzoefu wao kuhakikisha bendi yao inaingia katika soko la muziki kwa nguvu.

Bendi hiyo mpya tayari imerekodi nyimbo mbili, moja ikiwa imetengenezwa kwenye video na kusambazwa katika vituo mbalimbali vya teklevisheni.

Rocky alizitaja nyimbo hizo ni Nakuhitaji.ambao umerekodiwa katika video na Mtu wa Watu, lakini tayari wameandaa nyimbo sita.

"Tuna nyimbo sita zilizofaniwa mazoezi, mbili zimerekodiwa, nne bado hazijarekodiwa, zote zitasikika siku ya uzinduzi wa bendi yetu," alisema Mkurugenzi huyo.

Bendi hiyo ya Malaika inaongozwa na Mfalme Christian Bella, Katibu Mkuu ni Andrew Sekedia akisaidiwa na Emmanuel Karonji 'Totoo Zebingwa.

TANZANIA TOP MODELS WAINGIA KAMBINI RASMI.


SHINDANO la Taifa la mitindo lijulikanalo kama Tanzania Top Models waingia kambini rasmi jana katika hoteli ya JB Belmont iliyopo katikati ya jiji Dar es Salaam.

Kambi hiyo iliyowajumuisha jumla ya wanamitindo 20 ilianza rasmi kwa waandaji wao kuwapa somo warembo hao jinsi ya kuishi kwa upendo katika kipindi chote watakachokuwa kambini.

Akizungumza na wanamitindo hao mwenyekiti wa kamati hiyo Jackson Kalimkumtima aliwaasa warembo hao kuishi kwa kushirikiana na upendo kwa muda wote watakaokuwa pamoja katika kambi hiyo.

Jackson aliongeza kuwa ndani ya kipindi chote cha warembo hao watakachokaa kambini wapenzi wa fani ya mitindo nchini watapata fursa ya kutazama maisha ya wanamitindo hao kupitia kituo cha televisheni cha Clouds.

Naye mkufunzi wa wanamitindo hao Zakia Twahili naye aliwasisitizia swala la heshima miongoni mwa warembo hao kwa muda wote watakaokuwa pamoja.

Shindano hilo la mitindo limeijumuisha mikoa mbalimbali ya Tanzania ikiwemo Mwanza,Dodoma,Arusha,Dar es Salaam.

Wednesday, November 6, 2013

MISS UNIVERSE TANZANIA ATAMBA MOSCOW

 
MISS Universe Tanzania, Betty Boniface Omara ametamba katika maonyesho ya mavazi kwa warembo 85 wanaowania taji la Miss Universe la mwaka huu mjini Moscow.

Katika mashindano hayo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Vegas Mall, vazi la Betty lililobuniwa na mbunifu anayekuja kwa kasi nchini, Mwanakombo Salim, lilipendwa na mashabiki wengi na anamatarajio makubwa kushinda taji hilo wakati wa fainali za mwaka huu zilizopangwa kufanyika Jumamosi.

Vazi hilo limechorwa na wasanii wa Tingatinga, Said Kambili na Mimus, michoro ambayo ni maarufu nchini iliyoasisiwa na msanii maarufu wa zamani, hayati Edward Tingatinga. Vazi hilo hilo mbali ya kudumisha utamaduni wa Tanzania, pia limechorwa michoro mbali mbali ya kuvitangaza vivutio vya kitalii.

Vazi hilo pia lina nakshi za mkeka na miba ya  mnyama maarufu ajulikanaye kwa jina la Nungunungu. Vilevile pia umetumika kama njia ya kumuonyesha ndege Tausi kama inavyoonekana rangi za mkeka kwenye mkia na kilemba kichwani mwake.

Lengo kuu la nguo na michoro hii ni kutangaza kazi za mikono na  utalii wa Tanzania na miongoni mwa michoro iliyoonyeshwa ni Duma, Tembo na Twiga vilevile imeonyesha ndege na mali asili zipatikanazo Tanzania kama vile Tausi, vipepeo, mimea na Mlima Kilimanjaro.

Mashindano ya Miss Universe Tanzania 2013 yamedhaminiwa na hifadhi ya Taifa Tanapa. 



 

Wednesday, October 16, 2013

ANDAA KUKU WAKUOKWA

Vipimo:

 

*Kuku mzima        1


Tangawizi   na thomu          1 kijiko cha supu

Mtindi                                   3 vijiko vya supu

Rojo la ukwaju                     2 Vijiko vya supu

Pilipili mbichi                      1 kijiko cha supu

Chumvi                             kiasi

Bizari ya jiyrah (cummin poda) 1 kijiko cha chai

Bizari ya dania (coriander poda.1 kijiko cha chai

Paprika                            1 kijiko cha chai

Kungu manga ya unga      1/2 kijiko cha chai

Hiliki                                    1/2 kijiko cha chai

Mdalasini                              1/2 kijiko cha chai

Siki au ndimu                       3 Vijiko vya supu
 
 
 
 
 * Ukipenda muache na ngozi bila ya kumchuna au mtoe ngozi.
 
 
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
 
 
1.  Changanya tangawizi na thomu, pilipili mbichi pamoja na vitu vyote vingine katika kibakuli.

2.  Mpasue kuku kidogo (slit) kila mahali kuweka njia ya kuweka huo mchanganyiko wa rojo la kuvumbika.

3.  Mtie hilo rojo kila sehemu na muacha avumbike (marinade) kwa muda wa masaa mengi katika friji.

4.  Paka mafuta kidogo katika treya umuweke kuku, kisha mchome katika oveni moto wa 450ยบ kwa muda wa dakika 45 hadi awive.

5.  Mtoe na umuweke katika sahani ya kupakulia ukipambia na saladi upendavyo.
 

Thursday, October 10, 2013

ROSE NDAUKA AKANA KUWA NA UJAUZITO WA MTARAJIWA WAKE.

Mwigizaji wa filamu Bongo Rose Ndauka akana kuwa na ujauzito huku Mtarajiwa wake Malick Bandawe akiwa akidai anafanya kila awezalo ili Rose aenjoy katika kipindi hiki cha ujauzito.

Na Mtarajiwa wake huyo ambaye naye pia ni Msanii wa Bongo fleva alipoulizwa kuhusu Ndoa alisema anasuburia  mpaka atakapojifungua mana kwa imani ya dini yake haruhusiwi kuoa mke ambaye ni mjamzito.

Zifuatazo ni baadhi ya picha wakiwa katika Hotel yenye hadhi ya Nyota tano.