Tuesday, June 18, 2013

KABABU ZA KUCHOMA.

Leo katika upande wa mapishi nimekuandalia Kababu za kuchoma japo watu wengi wamezoea za kukaanga.
Kababu hizi ni zuri na hazina mafuta mengi
.

Mahitaji
Nyama ya kusaga                                         1kilo
Tangawizi na saumu iliyosagwa                  1 Kijiko
Chumvi                                                         kisia
Kitunguu maji kilichosagwa                        1Kikubwa
Yai                                                                1
Chenga za Mkate (bread crumbs)                1  Kikombe
Pili pili manga ya powder                            2 Vijiko
Bizari ya pilau  ya powder  (cummin)         2 Vijiko
Mafuta                                                          1/4kikombe
(ya kunyunyizia baada ya kupanga kababu) 
       
Namna ya kuandaa.
Anza kuandaa yai kwa kuipanua kisha weka kwenye bakuli kubwa kiasi.
 
Chukua nyama changanya  na viungo vyote pilipili,binzari,chenga za mikate,vitunguu tangawizi na chumvi kiasi.

Mchanganyiko wako ukishachanganyika vizuri anza kutengeneza umbo la kababu

Unaweza utengeneza muundo hata kama wa yai ambao umezoeleka.

Kisha vipange vipande vyote katika sinia ya kupikia katika jiko la oven.

Baada ya hapo kababu za kuchoma zitakuwa tayari na unaweza kutengeneza Saladi upendayo kwaajili ya mlo wako.

Chakula hiki unaweza kula wakati wowote na kinywaji upendacho.

No comments:

Post a Comment