Wednesday, July 24, 2013

FATUMA WA SEGERE AZIKWA LEO BAGAMOYO


Aliyekuwa mwimbaji wa wa kundi la Segere maarufu kwa kupiga nyimbo za kizaramo Fatuma Rajab atarajiwa kuzikwa leo katika kijiji  chao kilichopo wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani, imefahamika




Akizungumza na mtandao huu Meneja wa bendi ya Segere bwana Masharubu alisema marehemu alifariki jana katika hospitali ya Muhimbili na alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kifua kwa muda yaliyopsababisha hadi jana kifukia umauti wake.

Mwimbaji huyo aliyekuwa machachari na mwenye ustadi wa kuimba nyimbo za kizaramo alipitia bendi mbalimbali lakini alipata maarufu zaidi pale alipoimba wimbo wa Segere namba mbili na kuchukua nafasi ya Siza Mazongela aliyekuwa amejiengua katika kundim hilo.

Inna lillah waina ilaihi raajiun.


KELLY ROWLAND ANUSURIKA KUFA MAJI

Mwanamuziki wa miondoko ya R&B, Kelly Rowland ameokolewa kwenye bahari mara baada ya kukwama baharini kwa masaa 12.

Rowland akiwa na watu wengine kadhaa walikutwa na kisanga hicho wakati wanashuhudia maonyesho yaliyofanyika ndani ya boti moja mnamo siku ya Ijumaa asubuhi (July 19th) na gafla hali ya hewa ikabadilika na kusababisha mawimbi makali.

Kepteni wa boti hiyo alipatwa na wasi kutokana na hali ilivyobadilika, ila kepteni wa wa boti ya TowBoat U.S. aitwaye Noah Santos alifanikiwa kumuokoa kila mmoja aliyekuwa kwenye boti hiyo akiwemo mwanamuziki huyo wa ngoma ya “Sail On”.

Santos alisema “kila mmoja alikuwa anatetemeka.” Na baada alipokea asante ya moja kwa moja toka kwa Kelly Rowland:

“Tulitoka naye siku inayofuata nikiwa na mke wangu kisha akatununulia chakula cha usiku. Aliniambia kwamba mimi ni shujaa wake.”


Mpaka sasa aakuna kauli yoyote toka kwa Kelly Rowland au timu yake kutokana na tukio hilo.

Hebu cheki picha ya Kelly akiwa na muokozi wake, Noah Santos..