Thursday, January 24, 2013

SABABU ZA KUMSWALIA MTUME IKIWA LEO NI MAULID DAY

  Assalam alleykum jamia,leo ni siku ya Maulid ni katika sikukuu bora kwetu sisi waislamu ikiwa ni siku yakuzaliwa mtume wetu Mohammed.
 
 Lakini inawezekana unajiuliza kwanini basi tumswalie Mtume صلى الله عليه وآله وسلم? Jibu la swali hakika ni refu sana itaweza kuwa ni makala ndefu au kitabu kizima cha mas-alah haya. Lakini tutafupisha.
    1. Kumtukuza Mtume wa mwisho;

Kumswalia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ni katika kumtukuza kwani yeye ndiye Mtume wa mwisho, na hii ni neema kwetu Ummah wa Kiislamu kujaaliwa sisi kuwa yeye ndiye Mtume wetu. Na Allaah سبحانه وتعالى Ametuambia kuwa sisi ni Ummah bora kabisa. Bila ya yeye tusingeliweza kupata uongofu kamili (Qur-aan) na mafunzo ya Sunnah ambayo yametutoa kizani na kutuingiza katika nuru.
    Na ikiwa Allaah سبحانه وتعالى Mwenyewe Amemtukuza kwa kumtofautisha na Mitume mingine yote, kwani wote Amewaita kwa majina yao katika Qur-aan isipokuwa Mtume Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم pekee Amemwita aidha 'Ee Nabii', Ee Mtume. Basi sisi kumswalia ndio mojawapo ya njia ya kumtukuza.

2.    Ni ibada kwetu;
   Kwa vile ni amri kutoka kwa Mola wetu kama tulivyoona katika aya hiyo ya juu, na ndio maana tunamswalia mpaka kwenye Swalah zetu za fardhi na za Sunnah, bila ya kumswalia Swalah haikamiliki.

 3.    Rahma kwetu kupata fadhila na thawabu zaidi;
    Binaadamu kila siku ana makosa hata awe anafanya ibada vipi, kwa hiyo ni neema kwetu kuzidishiwa fadhila kwa kutekeleza vitendo vya Sunnah fulani ili kujiongezea thawabu na daraja ya Pepo kwani hakuna mtu asiyependa ziada ya neema.

 Fadhila ya Kuswaliwa na Allaah سبحانه وتعالى mara kumi

 عنْ عبد اللَّه بن عمرو بن العاص ، رضي اللَّه عنْهُمَا أنَّهُ سمِع رسُول اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم يقُولُ : (( من صلَّى عليَّ صلاَةً ، صلَّى اللَّه علَيّهِ بِهَا عشْراً))   رواهُ مسلم
Imetoka kwa 'Abdullaah ibn 'Amru ibn Al-'Aasw رضي اللَّه عنْهُمَا kwamba kamsikia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم anasema, ((Atakayeniswalia Swalah moja Allaah Atamswalia (Atampa rahma Zake) mara kumi)) [Muslim]

  Maana ya Swalah ya Allaah سبحانه وتعالى na Malaika Wake

Swalah ya Allaah سبحانه وتعالى kwa waja Wake ni: Rahma na kuwasifu kwa Malaika.
Swalah ya Malaika kwa Waumini ni:

Du'aa na kuwaombea maghfirah.
  Kupata daraja ya Pepo karibu naye Mtume صلى الله عليه وآله وسلم:

عن ابن مسْعُودٍ رضي اللَّه عنْهُ أنَّ رسُول اللَّهِ صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم قال : (( أَوْلى النَّاسِ بي يوْمَ الْقِيامةِ أَكْثَرُهُم عَليَّ صلاةً)) رواه الترمذي وقال : حديثٌ حسنٌ

Imetoka kwa ibn Mas'uud رضي اللَّه عنْهُ kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema, ((watu wa mwanzo kwangu (watakaokuwa karibu yangu)  siku ya Qiyaamah ni wale wanaoniswalia sana)). [At-Tirmidhy na kasema ni Hadiythi Hasan]

Vile vile kumuombea Du'aa, mfano du'aa baada ya adhaan ni fadhila kwetu kuwa atakayefanya hivyo atakuwa miongoni mwa atakayeombewa Shafa’ah na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم siku ya Qiyaamah.
4.    Kudhihirisha mapenzi yetu kwake ;

Muumini ni yule mwenye kumpenda khaswa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kabla ya kupenda chochote hata nafsi yake kwani ilipoteremka Aayah hii:

((النَّبِيُّ أَوْلَى بِالْمُؤْمِنِينَ مِنْ أَنفُسِهِمْ))  
((Nabii ni bora zaidi kwa Waumini kuliko nafsi zao)) [Al-Ahzaab: 6]

'Umar رضي الله عنه  alisema kuwa yeye anampenda Mtume kuliko chochote ila nafsi yake. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akamuambia 'Umar kuwa hadi ampende hata kuliko nafsi yake ndipo yatakapothibitika mapenzi yake, naye 'Umar akakubali kuwa anampenda kuliko hata nafsi yake. Kwa hiyo na sisi Waumini tuwe na mapenzi makubwa ya kumpenda na dalili mojawapo ni kupenda kumswalia na kufuata aliyokuja nayo na kujiepusha na aliyotukataza nayo ya uzushi (bid’ah) na mengine.

 5.   Kumswalia kwetu ni thawabu alizokwishaahidiwa;
   Allaah سبحانه وتعالى Amekwishamuahidi Mtume Wake kuwa atapata malipo mengi yasiyokatika:

((وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍ))

((Na kwa hakika wewe una malipo yasiyokatika)) [Al-Qalam: 3]
   Mbali ya kuwa ni malipo yake kwa sababu ya Utume wake na kufikisha ujumbe kwa tabu na mashaka, vile vile kumswalia kwetu kila siku katika Swalah zetu kila mara, na kuswaliwa na Ummah mzima wa Kiislamu tokea Utume wake hadi siku Qiyaamah ni mojawapo ya kuthibitisha kauli hiyo ya Allaah سبحانه وتعالى.

  Mwisho kama ulivyosema kuwa sisi ndio tuliokuwa njia panda na tunaohitaji kuombeana, bila shaka tunahitaji kufanya hivyo, na kwa hiyo pia kumswalia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ni kutuzidishia uzito wa mizani zetu za mambo mema na kufanya nyepesi mizani za mambo maovu.
Wa Allaahu A'alam

LULU KUACHIWA KESHO KWA DHAMANA


Taarifa za uhakika nilizozipata kwa sasa ni kwamba kuna uwezekano mkubwa mwigizaji Lulu akatoka kwa dhamana kesho january 25 2013.
     Uhakika wa Lulu kupata dhamana ulikua jana jumatano january 23 lakini ikawa imeshindikana kutokana na kuahirishwa kwa sababu jaji alipata dharura na pia kiwango cha pesa za dhamana kilikua hakijatimia.
     Chanzo cha kuaminika kilichoongea na millardayo.com kimesema dhamana ya kumtoa Lulu ambae amekua chini ya ulinzi kuanzia April 2012 ni milioni 20 za kitanzania.
      Lulu amekua akishikiliwa kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya mwigizaji Steven Kanumba, endelea kuipitia millardayo.com kwa stori zaidi.


SOURCE :www.millardayo.com

Wednesday, January 23, 2013

AY AWEKWA KWENYE JARIDA LA HESHIMA KENYA

AY ambaye jina lake halisi ni ABWENE YESAYA ana mengi aliyoyafikia na kumfanya apate heshima.Tukianza na tuzo za chanel O aliyoipata mwaka jana(video bora ya Afrika) kwa wimbo wake"i dont wanna be alone".AY ndie msanii wa Tanzania ambaye video zake zinachezwa kwenye tv za kimataifa kama speak with your body,part zone
Pia anang'ara kwenye video aliyoshirikishwa na msanii wa nigeria Goldie Harvey"skibono".Tayari ana wimbo uliokamilika aliofanya na Sean Kingston,na pia ana kampuni yake inaitwa UNITY ENTERTAIMENT inaendelea kukua kw sasa ikiwa na wasanii kama Ommy Dimpozi,Feza Kessy na Stereo kwenye roaster yake.

PRODUCER BAB CHIDY WA MY RECORDS NA UJIO WAKE MPYA

        Said Abdullah a.k.a Bab chidy ni producer ambae anafanya kazi katika studio 'my records' chini ya Boss wake Mo racka,mwaka jana alishatengeneza nyimbo ya flora mvungi na nisha wa bongo movie wakishiriana na Mo racka,ngoma inaitwa sinaga.Na sasa anawataka wapenzi wa muziki wakae tayari kwa ujio wake wa project zake zake mpya kwa mwaka huu.
              kutoka kushoto ni Bab Chidy,Lamar pamoja na Cyril
                                                                hapa akiwa studio
                     Hapa akiwa na Boss wake Mo Racka(kushoto).

NYOTA WA POP SHAKIRA AJIFUNGUA

    Mwanamuziki Shakira Mebarak amepata mtoto wa kiume huku mashabiki wakisema alipendeza sana na ujauzito wake.Mzazi mwenzake,Gerard Pique alitangaza kuwa wamepata mtoto wa kiume waliyempa jina la Milan Pique Mebarak ambapo alisema jina hilo lina maana ya Dear(mpenz).

BIG BROTHER AFRICA YAANZA KUPOKEA MAOMBI

   Lile Shindano la Big Brother Africa  ikiwa ni msimu wake wa8 linatarajia kuanza mwezi May mwaka huu.
   Na kwa vijana mwenye umri kuanzia miaka21,wacheshi,wavumilivu na wanaovutiwa na shindano hilo wana nafasi zuri ya kuanza kujaribu bahati zao.
   Mwaka huu nchi 14 za Afrika zitashiriki na nafasi ya Liberia itachukuliwa na Ethiopia sababu ni kutaka kushirikisha nchi nying zaid, nchi kama Angola,Boswana,Ethiopia,Ghana,Kenya,Malawi,Namibia,Nigeria,Sierra Leone,South Africa,Tanzania,Uganda,Zambia na Zimbambwe.
    Fomu za kujiunga zinapatikana www.Africamagic.tv/bigbrother na pia unaweza kuzipata katika ofisi za Multichoice katika nchi zote 14 kuanzia Mwezi wa Februar1 2013.
      Na litaanza rasmi Jumapili tarehe 26 may amapo washiriki watakaa katika jumba la Big Brother Africa kwa siku 91.
  

PETER WA 'P SQUARE' APATA MTOTO WA PILI

    Peter Okoye wa kundi linaloundwa na ndugu wawili Peter n' Paul(p square)na mkewe jana wamebahatika kupata mtoto wao wa pili wa kike waliyempa jina la'Aliona' mtoto huyo alizaliwa huko San Francisco nchini Marekani ambako Peter yuko nchini humo kwa mapumziko ya Familia yake amezibreak good news hizo kwa kuweka picha kwenye mtandao wa Instagram akiwa hospital bega kwa bega na mke wake ambapo kwenye picha ya juu ameandika'thanks u Lord...am the new Daddy in Town....And she is so beautiful and adorable.
   Peter akiwa na sura ya fuhara baada ya kupata mtoto wake wa pili.Na pia ana mtoto mwingine wa kiume ambae ndo mtoto wa kwanza kwake na mkewe aitwae Cameron.

 
ameandika:Mother and Child are perfectly fine...thank u God
 
 
 

 
 

Tuesday, January 22, 2013

SHILOLE NA STYLE MPYA YA NYWELE

     Bongomovie na msanii wa bongofleva Zuwena au Shilole au 'Mtoto mzuri amebadili mtindo wa nywele kwa kukata nywele na kuweka blich sehem ya kati(kiduku).Shilole alisema kuwa alikata kuwa alikata nywele siku ya jumapili ikiwa ni muonekano wake mpya kwa mwaka huu 2013.

MSONGO YAPATA MWANAMUZIK MPYA

Waimbaji wa bendi ya Msondo Ngoma wakiwajibika katika onyesholake maalum la kumtambulisha mwimbaji wao mpya Othumani Kambi(wa pili kulia)wengine ni Hassan Tx Moshi(wa kwanza kushoto)akifuatiwa na Eddy sana na Juma Katundu.Onesho hilo lilifanyika katika ukumbi wa Max Bar Ilala Bungoni.


Mashabiki wa Bend ya msondo wakicheza kwa furaha wakati wa onesho hilo

Monday, January 21, 2013

MAZUNGUMZO UWANJA WA NDEGE

    Mama Salma Kikwete(wa kwanza kulia) akibadilishana mawazo na Mke wa Rais wa Mali,Mama Toure Lobbo Traore aliyekutana naye uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Charles de Gaulle jijini Paris Ufarasa baada ya kuwasili kwa ziara za Kiserikali ya siku tatu (picha na Ikulu)

KUKANYAGA BUSTANI IKULU

      Askari Polisi wakiwa wamewaweka chini ya ulinzi wakazi wa Dar es salaam wenye asili ya China,baada ya kuwakamata kwa kosa la kukanyaga bustani inayozunguka eneo la Ikulu kwa gari lao, jijini Dar es salaam juzi(picha na Yusufu Badi).

UKUTA WA UBUNGO WAANGUKA NA KUSABABISHA UHARIBIFU MKUBWA

    Leo alfajiri ukuta wa Stand ya mabasi yaendayo mikoani Ubungo jijini Dar es salaam umeanguka nakuzusha hofu kubwa kwa wasafiri.
    Inadaiwa kuwa watu wanne wamejeruhiwanhuku magari 24 yaliyokuwa yameegeshwa mahali hapo yakiharibiwa vibaya na ukuta huo.
    Kamanda wa Polisi wa mkoa wa kipolisi Kinondoni Charles Kenyela alipokuja eneo la tukio alisema chanzo cha ajalini mkandarasi aliyekuwa akibomoa ukuta bila tahadhari.
     Hizi ni baadh ya picha za tukio hilo kwa hisani ya mtandao wa global.




JUISI YA EMBE NA PASSION

  Juisi ya embe na passion ni juisi rahisi kuandaa na pia ni juisi zuri kiafya.Unaweza kutengeneza kwaajil ya nyumbani au unaweza kubeba kwaajil ya kazini kuliko kununua juisi ambazo zina kemikali ambazo sio nzuri kwa afya.
      Mahitaji
Passion fruit                                                            8

Embe                                                           6 za kiasi

Maji                                                                       kiasi

Sukari                                                                   kidogo

       Namna Yakuandaa.
1.   Kata passion fruit toa nyama weka mashine ya kusagia (blender) . Tia maji   kiasi kisha saga na uchuje .

2.   Saga embe na maji kidogo kisha changanya na juisi ya passion.

3.   Tia sukari kidogo  ikiwa tayari kwa kunywewa.

      Lakini unaweza kutumia mchanganyiko  wa maembe na ma'passion kula bila kusaga mana vinakazi moja katika mwili wako.
      Unapata vitamini na inakukusaidia kupata choo vizur na faida nyinginezo.
 

Sunday, January 20, 2013

FASHION YA VIATU KWA WANAWAKE

     Katika vitu ambavyo wanawake au wasichana wapenda mitindo wanaziangatia ni pamoja na viatu hasa vilivopo kwenye vinavyoenda na wakati.
     Kuna viatu kwaajili ya harusi,kazi,mitoko ya jion.na sehem nyenginezo.Vipo virefu na flat.
          Vifuaatavyo ni baadhi ya viatu vyakisasa kwa wasichana