Saturday, January 19, 2013

SIKU YA MASTAA WA FILAMU TANZANIA YAKARIBIA


 Wasanii wa filamu nchini wanatarajia kufanya tamasha kubwa lililopewa jina la 'siku ya mastaa wa filamu Tanzania'.
  Tamasha hilo litafanyika tarehe 26 mwezi huu wa kwanza kwenye viwanja vya Dar Live jijini Dar es salaam.Lengo ikiwa ni kuchangia ofisi za shirikisho la filamu Tanzania(TAFF) ambapo kutakua na burudani mbalimbali.
   vikundi vitakavyotoa burudani ni pamoja na bendi ya Twanga Pepeta,Tunda man,Shilole,Snura,Kitale,Joti,Mpoki na wengineyo pamoja na wasanii wote wa filamu wanaounda Bongo Movie.

1 comment: