Sunday, January 13, 2013

HATUA ZA KUKUWEZESHA KUTIMIZA MALENGO 2013


       Habari za mwaka mpya mfuatiliaji wa blog yangu...hongera kwa kuchaguliwa kuuona mwaka mingine wa 2013,ni jambo la kushuruku na kuongoza juhud zaid katika shughuli zetu za kila siku.

       Wengi tulikuwa na malengo mwaka2012 lakini tulifanikiwa kiasi gani? kwanini haikuwa kwa 100%? kikwazo ni nini? inawezekana hukujua njia sahihi yakupita au wewe ulikuwa adui wa ndoto zako.

     Leo tuangalie hatua sahihi zakutuwezesha kufikia malengo au ndoto zetu tulizonazo.
Anza na moja;
    Unaweza kuwa na ndoto nyingi ambazo unatamani zikamilike mwaka huu lakini ni vizuri aanze na moja,hii itakusaidia kufikiria zaidi na kufanikiwa kwa urahisi.
Amini utafikia malengo;
    Adui wa kwanza wa ndoto zako unaweza kuwa wewe mwenyewe kwa unajipuuza au kujikatisha tamaa katika lile ambalo umeamua kufanya.amini wazo lako ni zuri na ni kubwa .
Omba ushaur;
    Unachotaka kufanya chochote lazima kuna watu ambao tayari wamefanya na wamefanikiwa,hivo ni vizuri kuomba ushauri kwao ili iwe rahisi kujua njia yakupita.Usiogope kuonekana hufahamu ni njia nzuri yakujifunza.
Badilisha mfumo wa maisha;
     Inawezekana ukawa na matumizi mabaya au huna mpangilio mzuri wa pesa zako.sasa ni wakat wakubadilika na kuanza kujinyima vitu ambavyo si vya lazima ili kuweka akiba.Hii itakusaidia kuwa na matumizi mazuri hasa kwa wenye ndoto za biashara.
Weka muda wakutimiza malengo;
     Mfano; unahitaji kufungua biashara weka akiba kwa muda sahihi.Panga kama ni miezi mitatu au sita ikiisha niwe nimetimiza kiasi fulani kwaajili ya kuanza kutimiza ndoto yangu.
Waambie wengine kuhusu malengo yako;
      wapo watu waliokuzidi umri,unaowaamini,kaa nao waambie kile unachofikiria kufanya waeleze kwa kina.Wanaweza kuwa wazazi.mke,mume au ndugu hata rafiki unaweza kupata jambo jipya kutoka kwao katika kuboresha ndoto zako.
Kua mgumu kukata tamaa;
       Muda uliotegemea kutimika ndoto yako umepita na hujakamilisha,usikate tamaa jipe moyo jipange upya fikiria wap ulikosea.
 Mtegemee mungu;
     Zote nilizokuelezea ni njia lakini mtegemee mungu,muombe katika yote ambayo unataka yatimie mana bila yeye hata 2013 tusingeweza kufikia.tchaoo

No comments:

Post a Comment