Thursday, January 17, 2013

NYAMA CHOMA YA NG'OMBE NA VIAZI

 
Nyama choma ni chakula kizuri ambacho unaweza kula wakati wa mchana au jion.Unaweza kuandaa chakula hiki katika mlo wako wa leo. ni rahisi kuandaa.

       Mahitaji
Nyama ya ng'ombe  bila kuikata stek(pande kubwa)   1/2 kilo

Viazi vilivyomenywa na kukatwa duara(sles)              4 vikubwa

Kitunguu swaum na tangawizi iliyosagwa                   2  vijiko vya chakula

Pilipili mbichi iliyosagwa                                            1kijiko cha supu

Mtindi (Yoghurt)                                                       1/2 Kikombe cha chai

Pilipili manga ya unga                                              1kijiko vya chai 

Bizari ya pilau ya unga                                            2vijiko vya chai


Chumvi                                                                   kiasi
 
 Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

1.  Changanya kitunguu swaum, tangawizi, chumvi, pilipili manga, pilipili mbichi, mtindi na bizari ya pilau katika kibakuli kidogo.

2.    Ichanje chanje nyama upate kuingiza mchanganyiko huo wa masala, kisha tia kidogo kidogo katika hizo sehemu wazi katika nyama na uroweke pande la nyama kwa muda  wa nusu saa
       
       Andaa jiko la mkaa liwe na moto kias weka wavu unaotumika kuchomea au jiko la kuchomea nyama weka nyama na iache kwa muda wa saa1.
 
  3.  Au unaweza kutumia oven,liweke katika trea ya kupikia ndani ya jiko (oven). Ifunike kwa jaribosi ya kupikia (foil paper) na ipike katika moto mkali 400º- 450º kwa muda wa saa1.

4.    Karibu na kuwiva, vitie viazi chumvi na pilipili manga kidogo na  umwagie juu ya nyama na uendelee kupika hadi viazi viwive pia.

5.    Epua ikiwa tayari kuliwa.Chakula hiki unaweza kula na mikate,salad au aina yeyote ya juisi au kinywaji ukipendacho.



 

  

 

No comments:

Post a Comment