Saturday, November 9, 2013

MASHAUZI KUONGOZA UZINDULIZI WA MALAIKA HIVI KARIBUNI.

BENDI ya muziki wa taarabu ya Mshauzi Classic, Cassim Mganga na Dully Sykes, watasindikiza uzinduzi wa bendi mpya ya Malaika utakaofanyika Novemba 15, mwaka huu katika ukumbi wa Mzalendo Pub, Kijitonyama, Dar es Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa bendi hiyo, Michael Rocky, alisema tayari walikubaliana na bendi na wasanii hao kushiriki katika uzinduzi wao.

"Tuliwaomba kama wasanii wenzetu, walikubali na kutuahidi kutoa burudani nzuri katika onesho hilo maalumu la kuzaliwa kwa bendi mpya," alisema.

Alisema wasanii hao, ni miongoni mwa wasanii wanaopendwa na mashabiki wa muziki kutokana na tungo zao kuwa na ujumbe mzuri.

Rocky ambaye aliwahi kuiongoza Akudo Impact kwa mafanikio, alisema watatumia uzoefu wao kuhakikisha bendi yao inaingia katika soko la muziki kwa nguvu.

Bendi hiyo mpya tayari imerekodi nyimbo mbili, moja ikiwa imetengenezwa kwenye video na kusambazwa katika vituo mbalimbali vya teklevisheni.

Rocky alizitaja nyimbo hizo ni Nakuhitaji.ambao umerekodiwa katika video na Mtu wa Watu, lakini tayari wameandaa nyimbo sita.

"Tuna nyimbo sita zilizofaniwa mazoezi, mbili zimerekodiwa, nne bado hazijarekodiwa, zote zitasikika siku ya uzinduzi wa bendi yetu," alisema Mkurugenzi huyo.

Bendi hiyo ya Malaika inaongozwa na Mfalme Christian Bella, Katibu Mkuu ni Andrew Sekedia akisaidiwa na Emmanuel Karonji 'Totoo Zebingwa.

No comments:

Post a Comment