Monday, August 26, 2013

JINSI YA KUANDAA KATLES ZA SAMAKI


 

Viazi    5 kiasi

Tuna    2 vikopo

Karrot 1

Pilipili             Nusu

Thomu          ½ kijiko cha chai

Pilipili          kiasi

Chumvi        kiasi

Ndimu         kiasi

Unga wa ngano     ½ kikombe

Yai              1

Mafuta ya kupikia        Kiasi      

                                                               

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA

1.      Menya Viazi uvichemshe na chumvi.

2.      Vikiwiva vichuje maji, viponde ponde, vilainikie – weka kando

3.      Chuna karrot ziwe kama chicha, kata pilipili mboga  nyembamba nyembamba,   fungua vibati vya Tuna kamua majia yake mwaga. 

4.      Changanya Tuna, karrot, pilipili mboga, thomu, pilipili kali, chumvi, ndimu, kisha uchanganye na viazi ulivyoviponda. Hakikisha vimechanganyika vizuri.

5.      Tengeneza vidonge kiasi unachotaka na kata umbo unalopenda kama la yai au duwara ukimaliza weka pembeni.

6.      Changanya unga na maji uwe mzito mzito tena uchanganye vizuri na yai.

7.      Weka karai katika moto, mimina mafuta kama ya maandazi, kisha chukua vidonge chovya katika unga uliochanganywa yai  na utumbukize ndani ya mafuta yaliopashika moto vizuri.

8.      Ziwache mpaka zibadilike rangu, uzitoe. Tayari kwa kula. 

No comments:

Post a Comment