Thursday, March 21, 2013

FILAMU YA MWISHO YA KANUMBA YAZINDULIWA SIKU YA KUMBUKUMBU YAKE YA MWAKA1

 
Kanumba-Movie-ya-mwisho-kabla-ya-kufariki
     Tarehe 7/4/2012 ndiyo siku ambayo marehemu Steven Kanumba alifariki dunia, kwenye kumbukumbu yake mwaka huu kutakuwa na uzinduzi wa filamu ya mpya ya Kanumba titled “Love and Power”.
      Hii ndiyo movie ya mwisho Kabisa ya Kanumba ambayo siku hiyo kutakuwa na misa ya kumuombea kwenye kanisa la Kimara na baada ya hapo mambo yatahamia Leader’s Club. Hapo leaders kutakuwa na uzinduzi wa movie hiyo kwa watu wote ambapo hakutakuwa na kiingilio.

       Seth Bosco ambaye ni mdogo wake Steven Kanumba ameelezea siku hiyo kama ifuatavyo,”Itakuwa ni siku ambayo tutatimiza mwaka mmoja baada ya mpendwa wetu Kanumba kufariki dunia, kumbukumbu yake itaenda pamoja na misa ya kuombea na baadaye uzinduzi wa filamu yake moya inaitwa Power and Love. Watu wote mnakaribishwa kwasababu hakutakuwa na kiingilio chochote siku hiyo”

No comments:

Post a Comment