Saturday, March 23, 2013

MICHAEL JORDAN ADAIWA KUKWEPA MAJUKUMU

 



Sakata la Michael Jordan la kudaiwa kukwepa kubeba majukumu
ya kumlea mtoto wake limechukua sura mpya baada ya mama
 wa mtoto huyu, Pamela Smith kupeleka maombi maalum kwa Jaji
 wa kesi hii kumtaka atoe amri ya kufanya vipimo vya DNA kati
 ya Jordan na mtoto wake.
Hatua hii imekuja baada ya Jordan kukataa kuwahi kumlea
 mtoto huyu ambaye anatambulika kwa jina Grant Taj Reynolds
aliyezaliwa mwaka 1996
.
Katika nyaraka mpya ambazo Pamela Smith ameziwasilisha,
mwanamama huyu ameandika kuwa ana uhakika kuwa
Michael Jordan ndiye baba halisi wa mtoto wake kwa sababu
 hesabu zake zinaonyesha kuwa miezi 9 kamili kabla ya kujifungua
 mtoto wake alilala na nyota huyu wa zamani wa mpira
wa kikapu.
Bado Jaji ajatoa maamuzi mpaka sasa kuhusiana na hatua
 ambayo itaamua hatma ya nyota huyu na familia mpya ambayo
inawezekana kuwa ni ya kwake.


No comments:

Post a Comment