Sunday, March 3, 2013

IRENE UWOYA NDANI YA LAST CARD

 

iRENNE UWOYA

Irene Uwoya mwigizaji wa filamu Swahiliwood.
     MWANADADA mwenye mvuto katika tasnia ya filamu Bongo Irene Uwoya amerudi tena kwa kuingia na filamu ya Last Card msanii huyo alikuwa kimya kidogo kwa ajili ya maandalizi ya filamu na sasa ameingia na last card kazi anayoaamini kuwa itafanya vizuri katika soko la filamu kutokana na uzuri wa kazi hiyo kuandaliwa kwa umakini zaidi, Irene Uwoya ni moja kati ya wasanii wa kike wenye wapenzi wengi wa kazi za filamu nchini.

Filamu ya Last Card

Picha ya Filamu Last Card.
Irene uwoya
Irene Uwoya akiwa kajishika tama kwa pozi.
“Ninafungua mwaka kwa bonge la filamu, sitaki kuwaambia kilichopo ndani ya filamu ya Last card bali mtu akibahatika kuiona atasema mwenyewe kuwa kazi hiyo kwa nini imeitwa Last Card, ni kazi bora sana kwangu na wote tulioshiriki katika filamu na naweza kuwahakikishia wapenzi wa kazi zangu kuwa hii ni kiboko si ya kuikosa,”anajitamba Irene.
          Filamu ya Last Card inakutanisha Irene Uwoya na mwigizaji mwenye sifa za filamu za kimahaba nchini Baba Haji na kuifanya filamu kuwa na visa mikasa ya kuvutia zaidi, inasemeka kuwa Baba Haji ndio msanii ndio msanii pekee bingwa wa kuigiza filamu za mahaba Bongo mwenye uwezo wa kubembembeleza na kushawishi, pia katika filamu hiyo unakutana na wakali wengine kama Janeth Sospeter, Omary Barafu na wasanii wakali katika tasnia ya filamu Bongo, filamu hiyo inasambazwa na Steps Entertainment.

No comments:

Post a Comment