Saturday, March 2, 2013

RADO AJA NA FALL IN LOVE

 

Simon Mwakipagata
Rado mwigizaji wa filamu Swahiliwood.
FILAMU ya Fall in Love ya Simon Mwakipagata ‘Kaptorado’ inatarajia kumweka vizuri msanii huyo baada ya kubadilika katika staili yake ya uigizaji, Rado mara nyingi upendelea kuigiza filamu zinazomweka katika nafasi za kitemi lakini katika filamu ya Fall in love anaigiza kwa aina nyingine ya kimapenzi, Rado mwenyewe anasema kuwa amepanga kila anapotoa filamu amelenga kubadilika badilika kwa ajili ya kuhakikisha wapenzi wake wanapata filamu bora na za kuburudisha.



Rose Ndauka
Rose Ndauka pia yupo
Haji Salum

Mboto mchekeshaji mahiri naye yupo katika filamu Fall in Love.


 


  • Simon Mwakipagata

 
“Filamu yangu ya Fall in Love imekuja kivingine maana wapenzi wa filamu wamezoea kumuona Rado akiwa na misheshe mwanzo mwisho lakini humu ni mambo mazito ya kimaisha mahusiano na kila kitu, nilikuwa nimepanga mwaka uliopita nilifanya kazi kwa ajili ya watoto nikatoa filamu ya Maduhu nikishirikiana na watoto walioibuliwa na marehemu Kanumba, sasa nimerudi na watu wazima kielimu zaidi kupitia filamu ya Fall in Love,”amedai Rado.
Msanii huyo amejigamba kwa kusema kuwa kazi yake hiyo imeandaliwa kwa umakini zaidi jambo linalomfanya ajivunie filamu hiyo kwani amefanya kazi kubwa kuanzia uandishi wa muswada wake, huku pia akiwasifia waigizaji wake kuigiza katika kiwango cha juu, wasanii
walioshiriki katika filamu hiyo ni Rose Ndauka, Salum Haji aka Mboto mchekeshaji anayefanya vizuri katika filamu hasa sehemu za kuchekesha.



No comments:

Post a Comment