Thursday, August 15, 2013

EFRANCYAH AGEUKIA MUZIKI

Efrancyah Mangii ambaye ni muigizaji wa filamu ameamua pia kuingia katika muziki wa Bongofleva akitarajia kuimba mahadhi ya Afro pop.

Akizungumza na blog hii Efrancyah alisema kuwa kwasasa yupo katika mazoezi makali na wiki ijayo anatarajia kuingia studio.

Aliongeza kwa kusema kuwa atamshirikisha mwanamuziki mwingine lakini hakuwa tayari kuweka jina la msanii atakayemshirikisha kwa wakati huu.

Kuingia kwa Efrancyah kwenye tasnia ya muziki kunazidi kuongeza idadi ya wasanii wa filamu waliojitosa katika muziki pia kama vile Shilole, Aunt Ezekiel, Snura Mushi, Kingwendu, Bambo, Mzee Magari, na pia Wema Sepetu yupo mbioni kuachia wimbo wake.

No comments:

Post a Comment