Thursday, August 15, 2013

UTABIRI WA THEA HATIMAYE WATOKEA KWELI.

Mwigizaji maarufu wa filamu nchini Ndumbagwe Misayo(Thea) amesema kuwa ule msimu wa ma-miss kuvuma kwenye tasnia ya filamu umeshapita na waliokuwa wakitamba miaka michache iliyopita kwasasa hawasikiki tena au ni majina tu yamebaki lakini katika filamu hawaonekani tena.

 Miaka michache iliyopita Thea ambaye ni mmoja wa waigizaji wenye vipaji vya hali ya juu aliwahi kusema kuwa tasnia ya filamu imevamiwa na mamisi ambao wengi wao vipaji hawana.

 Akizungumza na blog ya Swahili world planet Thea aliyetamba na michezo kadhaa Kaole na sasa katika filamu alisema "Utabiri wangu unafanya kazi kwa sababu kwa sasa wale wasanii walioibukia kwenye mashindano ya u-miss wengi hawasikiki tena.

Wasanii wanatakiwa kutambua kuwa sanaa hii siyo lelemama yaani mpaka kufikia hapa tulipo tulifanya kazi ya ziada, tulisota sana kwenye vikundi"
Kwasasa Thea yupo location akishuti filamu mpya akiwa na Jacob Stephen(JB), Shamsa Ford na Bi. Hindu

No comments:

Post a Comment