Monday, August 12, 2013

SHAMSA: DINI HAIWEZI KUNIKOSESHA NDOA


Mwigizaji wa filamu maarufu Shamsa Ford 'Shamsa' akiri kuwa mpaka sasa hajajua ndoa yake itafungwa katika maadili ya dini ipi kutokana na kutofauti iliyopo.

Akizungumza na blog hii hivi karibuni Shamsa alisema ingawa vikao vya harusi tayari vimeanza lakini bado yeye na mchumna wake hawajajua kuhusu ndoa yao itafungwa kwa iman gan.
Shamsa alisema yeye ni muislamu na mumewe mtarajiwa Dickson ni Mkirsto lakini wanaamini tofauti hiyo haiwezi kukwamisha ndoa yao kwani wote wanaamini mungu ni mmoja.

"Mimi na Dickson kweli tupo katika dini tofauti lakini hiyo haiwezi kukwamisha lengo letu kwani mungu ni mmoja na ni jambo lakukubaliana mimi kumfuata au yeye kuja katika dini yangu"Alisema Shamsa.

Pia mwigizaji huyo alisema katika kuonyesha upendo kwake mchumba wake alifunga katika kipindi chote cha mwezi mtukufu wa ramadhani.


Shamsa aliongeza kuwa ndoa ni japo muhimu kwao kwa sasa pamoja na mtoto wa kike aitwaye Teddy ambaye anahitaji mapenzi ya baba na mama.

Ndoa hiyo ya imekuwa ikitajwa kuwepo na kuahirishwa mara kwa mara kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya Shamsa kutokua tayari kuolewa lakini sasa wameamua kufanya kweli.

No comments:

Post a Comment