Tuesday, April 30, 2013

BABA CHRIS BROWN AVUTIWA NA HUYU KUWA MKWE NA SI RIHANNA

 

Gazeti la New York Daily News limefanya Exclusive interview na baba mzazi wa mwimbaji staa Chris Brown na kutoa maoni yake kuhusu mahusiano ya kimapenzi ya mwanae na Rihanna RiRi.

Clinton Brown amesema “sioni maisha marefu kwa Chris Brown kuwa na Rihanna, sijawahi kupendezwa na kurudiana kwao, unajua ni lazima kwenye uhusiano wa kimapenzi uwe na mtu sahihi ambae ni hitaji la kweli na linaloweza kuwa lako kwenye maisha, lakini sio kama hivi”

Clinton amesema hapendi kutumia mifano lakini anadhani watu wameona mahusiano ya mastaa kama Whitney Houston, Michael Jackson, Amy Winehouse na wengine”

Kuhusu mrembo ambae angependa kuona anaolewa na mwanae, Clinton amemtaja Jordin Sparks kwa kusema “nimempenda Jordin, ni msichana mdogo lakini mwenye upeo mkubwa… ana akili na heshima

HAMMER Q AMSHUSHIA MKEWE KIPIGO KISA HASSAN TX MOSH

 Hammer Q akiwa na Mkewe siku ya harusi yao.
 
zifuatazo ni baadh ya picha za Salha akiwa na majeraha

Msanii wa Taarabu wa kundi la Five Star na kundi la Off Side Trick amempiga mke wake wa ndoa kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa mapenzi.
Salha mke wa Hammer Q ambaye pia ni msanii anayeunda kundi la Dar es Salaam Modern Taarabu alisema mumewe alianza kumpiga walipokuwa katika show ya kundi la Five Star iliyokua inafanyika Dar Live Mbagala jijini Dar es salaam.


Akizungumza na Clouds Fm kwa njia ya simu alisema amelazwa katika hospital baada ya kupigwa alisema walipokuwa Dar Live Salha alionana na Hassan Tx Mosh akamtambulisha kwa mumewe ambaye ndipo Hammer alipoanza kumpiga kwa kusema kwanini ametambulishwa.

"mimi sikuona tatizo kumtambulisha lakin baada ya hapo alitaka tuondoke tulipofika nyumbani kipo alipoanza kunipiga sana amenichana sana mgongoni,mikononi,usoni na hapa nimeshonwa nyuzi nyingi"

Baadh ya mashuhuda ikiwepo mwenye nyumba wao alisema walimsihi sana aache kumpiga mkewe lakini alisema yule ni mkewe na alilipa pesa hivyo hataki mtu aiingilie.

"watu walimsihi sana asinipige lakin alikataa alinipiga mpaka na jiko la uso na ameniharibia sana vitu vyang ndani kwang yani sijui kama ntaweza kurudiana tena mana si mara ya kwanza"

Lakini alipotafutwa Hammer Q alisema ilikua ni hasira na walikua wamelewa hivyo ni pombe tu.

Kesi imeshafika polisi na wazazi wa Salha wanafuatilia na Hammer Q hajulikani alipo mpk sasa.

Uongozi wa Blog hii unalaan vikali vitendo kama hivi mana ni unyanyasaji wakijinsia.

Endelea kufuatilia Blog hii kuweza kujua kitakachoendelea

Monday, April 29, 2013

TUNDAMAN ATOA YAMOYONI KUHUSU STYLE YAKE MPYA YA NYWELE



Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini ambaye pia ni mshiriki wa kundi la Tip Top Connection Tundaman ameamua kuongea ya moyoni baada ya baadhi ya mashabiki wake kuponda staili yake mpya ya nywele kupitia mitandao ya kijamii.
Akizungumza na gazeti hili Tundaman alitoa sababu zakuweka staili hiyo ya nywele ambapo alieleza kuwa mcheza sinema maarufu anayemuhusudu aitwaye Tom Po ndiye anaweka staili hiyo ya nywele siku zote.

Tundaman alisema amekua na muonekano wa kawaida kwa muda mrefu hivyo ameamua kuwa na mpya na hiyo ndiyo sababu iliyochangia yeye kuweka stail hiyo ya Tom Po .



"Nimekua na staili moja ya nywele siku nying hizo nimependa niwe na muonekano mpya  sababu nampenda sana Top Paul na mara nyingi naangalia filamu anazocheza na kwakua siwezi kuigiza kama yeye ndio maana nikaamua kuweka staili hii ili kuonyesha mapenzi yangu kwake"Alisema.

Aliongeza kuwa" Hata Lil Wayne alipoamua kuchora tatoo mwili mzima baadh ya mashabiki walimsema vibaya lakini sasahivi wamezoea na maisha yanaendelea hivyo kwang pia watazoea"

Hata hivyo alisema kuwa tayari ameshaitambulisha nyimbo yake ya 'wanaona haya' aliyoshirikiana na Chege na video wanaenda kuifanya katika jiji la Nairobi nchini Kenya.
 

Saturday, April 20, 2013

KAJALA AKIRI KUMKOSEA MAMA YAKE.


Kajala ametoka kukumbana na kashikashi katika maisha yake hivi karibuni, baada ya kusota jela takriban mwaka mmoja kutokana na kesi ya kutakatisha fedha iliyomwandama yeye na mumewe ambaye yuko jela.

Akizungumza katika kipindi cha ‘Take One’ kinachorushwa kila Jumanne na Clouds Tv, Kajala alisema alipokuwa jela alimkumbuka mama yake kwa mambo aliyokuwa akimwambia na kuanza kujuta kutokana na mateso aliyokutana nayo huko.
 
           “Mimi nilianza kumkumbuka sana mama yangu alivyokuwa akiniusia kutulia, ila mimi natoroka nyumbani nakwenda ninakotaka na kumuacha katika huzuni, ila nilipokaa jela niliona nini umuhimu wa mama, namuomba anisamehe sikujua nilitendalo,” alisema Kajala
 
Aidha, Kajala alisema katika familia yao, mama yake alikuwa ni mkali kuzidi baba yake, ambaye kila kitu walichotaka kufanya aliwaruhusu, ikiwa ni pamoja na kwenda katika majumba ya muziki, lakini mama yao alikataa na kudai sasa anatambua umuhimu wake.

           Aliwashukuru wote ambao walikuwa naye bega kwa bega hadi kufanikisha kutoka jela, huku shukrani za pekee akizimwaga kwa msanii mwenzake Wema Sepetu ambaye alimnusuru kufungwa jela miaka saba kwa kumlipia faini ya sh milioni 13.

Thursday, April 18, 2013

DAVINA APATA MTOTO WA KIUME



 
Msanii wa filamu nchini Halima Yahya 'Davina' amejifungua mtoto wa kiume katika Hospitali ya Agha Khan jijini Dar es salaam.
 Davina amejifungua jumapili katika hospitali ya Agha Khan na anamshukuru mungu amejifungua salama na amerudi nyumban kwa mumewe anayeishi naye sasa Tabata.
“Namshukuru sana Mungu nimejifungua salama, nilimwomba iwe hivyo. Kwa sasa namwomba Mola amjalie afya njema na maisha marefu mwanangu" Alisema.


 

LULU ATIMIZA MIAKA '18'



Lulu akimlisha keki mdogo wake

Akipakua chakula kwenye sherehe yake.
 

Tuesday, April 2, 2013

SUMATRA YATANGAZA VIWANGO VIPYA VYA NAULI


      Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini SUMATRA imetangaza viwango vipya vya nauli za mabasi ya masafa marefu, daladala katika jiji la Dar es Salaam, nauli za usafiri wa reli ya kati na bandari.
      Viwango hivyo vimetolewa kutokana na SUMATRA kufuatia maombi rasmi kutoka kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri na makampuni binafsi nchini kutokana ongezeko la gharama za uendeshaji.
       Ahmad Kilima ni Kaimu mkurugenzi mkuu wa SUMATRA amesema viwango vipya vimetolewa baada ya kufuata taratibu za kisheria na utendaji kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali katika kujadili na kupata maoni yao kuhusu ongezeko la nauli.
      Amesema SUMATRA imeongeza viwango vya juu vya nauli ya daladala kwa wastani wa asilimia 24.46 na mabasi ya masafa marefu viwango vimeongezwa kwa asilimia 20.3
Pia amesema ili kuhakikisha kuwa kuna uwiano kati ya viwango vipya vya nauli na ubora wa huduma ya usafiri, mamlaka imewataka wamiliki wa mabasi kutotumia wapiga debe katika kuuza tiketi za usafiri na kwamba watakaokaidi hatua za kisheria zitachukuliwa.
       Bwana Kilima amesema katika kufanya mapitio ya gharama mbalimbali za bandari na bahari kuu mamlaka imeridhia ongezeko la gharama kwa wastani wa asilimia 34.3 hivyo TPA wametakiwa kuboresha huduma kwa wateja kwa kuanzisha kitengo cha huduma kwa wateja .
        Hata hivyo ongezeko hilo la nauli limeenda sanjari na viwango vya nauli kwa usafiri wa abiria wa reli ya kati ambapo mamlaka imewataka abiria kukata tiketi na kupanda treni wakionyesha vitambulisho…
     Viwango vipya vya nauli vinatarajia kuanza kutumika kuanzia tarehe 12 Aprili 2013 ambapo nauli ya mwanafunzi itakuwa shilingi 200 na mtu mzima atalipa shilingi 400 kwa safari za mijini.