Tuesday, April 30, 2013

HAMMER Q AMSHUSHIA MKEWE KIPIGO KISA HASSAN TX MOSH

 Hammer Q akiwa na Mkewe siku ya harusi yao.
 
zifuatazo ni baadh ya picha za Salha akiwa na majeraha

Msanii wa Taarabu wa kundi la Five Star na kundi la Off Side Trick amempiga mke wake wa ndoa kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa mapenzi.
Salha mke wa Hammer Q ambaye pia ni msanii anayeunda kundi la Dar es Salaam Modern Taarabu alisema mumewe alianza kumpiga walipokuwa katika show ya kundi la Five Star iliyokua inafanyika Dar Live Mbagala jijini Dar es salaam.


Akizungumza na Clouds Fm kwa njia ya simu alisema amelazwa katika hospital baada ya kupigwa alisema walipokuwa Dar Live Salha alionana na Hassan Tx Mosh akamtambulisha kwa mumewe ambaye ndipo Hammer alipoanza kumpiga kwa kusema kwanini ametambulishwa.

"mimi sikuona tatizo kumtambulisha lakin baada ya hapo alitaka tuondoke tulipofika nyumbani kipo alipoanza kunipiga sana amenichana sana mgongoni,mikononi,usoni na hapa nimeshonwa nyuzi nyingi"

Baadh ya mashuhuda ikiwepo mwenye nyumba wao alisema walimsihi sana aache kumpiga mkewe lakini alisema yule ni mkewe na alilipa pesa hivyo hataki mtu aiingilie.

"watu walimsihi sana asinipige lakin alikataa alinipiga mpaka na jiko la uso na ameniharibia sana vitu vyang ndani kwang yani sijui kama ntaweza kurudiana tena mana si mara ya kwanza"

Lakini alipotafutwa Hammer Q alisema ilikua ni hasira na walikua wamelewa hivyo ni pombe tu.

Kesi imeshafika polisi na wazazi wa Salha wanafuatilia na Hammer Q hajulikani alipo mpk sasa.

Uongozi wa Blog hii unalaan vikali vitendo kama hivi mana ni unyanyasaji wakijinsia.

Endelea kufuatilia Blog hii kuweza kujua kitakachoendelea

No comments:

Post a Comment