Monday, April 29, 2013

TUNDAMAN ATOA YAMOYONI KUHUSU STYLE YAKE MPYA YA NYWELE



Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini ambaye pia ni mshiriki wa kundi la Tip Top Connection Tundaman ameamua kuongea ya moyoni baada ya baadhi ya mashabiki wake kuponda staili yake mpya ya nywele kupitia mitandao ya kijamii.
Akizungumza na gazeti hili Tundaman alitoa sababu zakuweka staili hiyo ya nywele ambapo alieleza kuwa mcheza sinema maarufu anayemuhusudu aitwaye Tom Po ndiye anaweka staili hiyo ya nywele siku zote.

Tundaman alisema amekua na muonekano wa kawaida kwa muda mrefu hivyo ameamua kuwa na mpya na hiyo ndiyo sababu iliyochangia yeye kuweka stail hiyo ya Tom Po .



"Nimekua na staili moja ya nywele siku nying hizo nimependa niwe na muonekano mpya  sababu nampenda sana Top Paul na mara nyingi naangalia filamu anazocheza na kwakua siwezi kuigiza kama yeye ndio maana nikaamua kuweka staili hii ili kuonyesha mapenzi yangu kwake"Alisema.

Aliongeza kuwa" Hata Lil Wayne alipoamua kuchora tatoo mwili mzima baadh ya mashabiki walimsema vibaya lakini sasahivi wamezoea na maisha yanaendelea hivyo kwang pia watazoea"

Hata hivyo alisema kuwa tayari ameshaitambulisha nyimbo yake ya 'wanaona haya' aliyoshirikiana na Chege na video wanaenda kuifanya katika jiji la Nairobi nchini Kenya.
 

No comments:

Post a Comment