Saturday, June 8, 2013

NYOKA AITWAE MATILDA AGUNDULIKA TANZANIA.


Nyoka aina mpya duniani mwenye magamba ya njano na nyeusi na macho ya kijani nyepesi, na mapembe mawili amegunduliwa huko Tanzania.


Na amepewa jina la mtoto wa miaka 7 aitwaye Matilda.

Matilda aligunduliwa nchini Tanzania maeneo ya kusini magharibi miaka miwili iliyopita na alitambulishwa mwezi uliopita kama aina mpya ya nyoka iliyojulikana katika jarida la Zootaxa.

Tim Davernport mkurugenzi wa shirika la hifadhi ya wanyama pori Tanzania alikuwa ni mmoja katika timu ya watu watatu waliomgundua nyoka huyo.

Nyioka huyo alipewa jina la mwanae Matilda mwenye umri wa miaka 5 kwasababu alikuwa akimpenda sana nyoka huyo na kumwangalia saa zote.

Katika miongo mitatu iliyopita ni aina za nyoka watatu tu waliogundulia katika bara zima la Afrika na kuanya utambuzi huo kuwa muhimu na wa nadra sana.

Shirika la wanayampori halisemi ni wapi hasa alikopatikana nyoka huyo ili kuzuia wawindaji wanaotafuta fedha . 

Imeandaliwa na:Christina Mokmirya 

BIKINI ZAPIGWA STOP MISS WORLD


Bikini ni vazi lililozoeleka kuvaliwa katika mashindano ya urembo likiwa vazi la ufukweni lakini tofauti na miaka yote mwaka huu waandaaji shindano la mrembo wa dunia wamesema  vazi hilo halitatumika kwenye shindani la hilo.

Wakieleza sababu za kutokutumika kwa vazi hilo ni taratibu za kimaadili kwa vile shindano hilo linafanyika kwa mara ya kwanza mashariki ya mbali katika nchi ya indonesia ambapo 90% ni waislamu.

Walisema badala yake warembo wote 137 watavaa vazi kuogelea la utamaduni ili kupunguza mtazamo tofauti wa kimadili kuhusu shindano  hilo.

Kwanza mara ya kwanza indonesia inakuwa mwenyeji wa shindano litakalofanyika baadaye september mwaka huuu

(source:the sun).

Thursday, June 6, 2013

MPIGIE KURA FEZA ABAKI KWENYE BIG BROTHER


Je leo umempigia kura Feza ili aweze kubaki kwenye jumba? kama bado Andika neno Feza kwenda 15456 au kupitia http://bigbrotherafrica.dstv.com/vote/

Tuesday, June 4, 2013

WANAUME SOMENI HAPA FAIDA ZAKUPIGWA VIZINGA NA WAREMBO

Vijana wengi tumekuwa tukilalamika kwamba mabinti wa siku hizi wana mizinga ya reja reja ten mikubwa.

Hili jambo ukiliangalizia katika “big screen” ni jambo ambalo linakufanya utafute hela if you really want to be with a girl of your dreams though sio lazima a girl of your dreams awe mpiga mizinga!!!!!
Jambo hili zuri nahisi vijana wengi hatujaligundua na badala yake tunalichukulia in a negative way na kubakia tunawalalamikia hawa mabinti, ila kumbe katika hali halisi wanatusaidia.
Maana katika hali ya kawaida lets say kama umeajiriwa somewhere, mshahara peke yake hautoshi kumkeep huyo binti unayemuita wa kisasa au wa mizinga! Sasa kulingana na mahitaji yake kuwa makubwa lazima utatafuta njia nyingine za kupata hela tuseme labda utawekeza mahali.

Lengo likiwa kuhimili mizinga ya huyo binti na kuendelea kumuweka karibu, ila mwisho wa siku unajikuta katika kuwekeza kwako una make faida zaidi ya hizo demands na kwa maana hiyo unakuwa na salio ambalo unaweza kujifanyia maendeleo yako mengine.
Ila kama huyo binti asingekuwa na hizo demands kubwa ungeridhika na mshahara wako, maana utakuwa unawatosha na mwisho wa siku hata kuwekeza mahali huwezi fikiria , na maendeleo yako bila shaka yatakuwa si sawa na yule anayemmiliki binti wa kisasa!!!!!!!!!!

Nahitimisha kwa kuwatia moyo mabinti wa kisasa waendelee na moyo wao huo huo wa kupiga mizinga tena mikubwa ili tutoke hapa tulipo kama Taifa!

Thursday, May 23, 2013

WANANDOA WA3 WALIOOANA SIKU 1 WASHEREKEA MIAKA 50 YA NDOA ZAO

Kusherehekea miaka 50 ya ndoa ni sherehe yenye furaha sana kwa kila waliofikisha miaka hiyo, zaidi ni pale unaposherehekea na rafiki zako wanne,
 
 ambao nao wananyanyua glasi kusherehekea sherehe yao wakiwa wanafikisha miaka hiyo hiyo ya ndoa zao, ila zaidi ni pale ambapo hao unaosherehekea nao, kama bahati walifunga  ndoa siku moja na wewe ndani ya kanisa moja.

 Norman na Mary Dickinson na Harry na Jean Winstanley, kutoka Flookburgh, Cumbria,  Alan na Anne Akrigg, kutoka Cark, Cumbria, wote walioana kwene kanisa la St John's lililopo  Flookburgh siku moja miaka 50 iliyopita mwaka 1963.

Tuesday, May 21, 2013

DAYNA AVUTIWA NA AFANDE SELE


Mwanamuziki  toka  mkoani  Morogoro  anayefanya  poa  kwa  sasa  na  ngoma yake  iitwayo  Leo  mwanadada  Dayna  Nyange  a.k.a  Mkali  wao,  amefunguka  na kumpigia  saluti
mwanamuziki  mkongwe toka  hapa  Morogoro Afande  Sele.

 '' kwa  kweli  siku  zote,  nimekuwa  nikimkubali  sana  Afande  sele  kwa  tungo zake  zenye  ujumbe,  lakini  kwa  wimbo  huu wa  Dini tumeletewa,  nampigia  saluti" Alisema Dayna na kuongeza kuwa,

 "Afande  ni  bonge  la msanii  na  huwa naskiliza  nyimbo  zake kwani  najuwa
nikiskiliza  nyimbo  zake  kuna  madini  napata,  lakini  sasa kaka  mkubwa  kwa  hapa  alipofikia  na kufikilia  kwa  kina juu  ya  wimbo  huu,  anastahili  kuwa mfalme wa  Rhyme,  waliompa  tuzo  hawakukosea".

 
Dayna ni mama wa mtoto mmoja na amewahi kutamba na nyimbo zake tofauti tofauti ikiwemo fimbo
ya mapenzi na nivute kwako aliyofanya na Barnaba.
 

HIKI NDICHO KILICHOMPATA MADAM RITHA


Akizungumza na Ijumaa Wikienda baada ya kuwa kimya muda mrefu ikielezwa kuwa alipata ajali hiyo kitambo, Madam Rita alisema kuwa kwanza kabisa anamshukuru Mungu kwani anaamini kila kitu kinachotokea chini ya jua kina sababu yake na hata alipopata ajali hiyo alimshukuru kwa kutoka salama.

Madam Rita aliendelea kueleza kuwa ajali hiyo aliipata katikati ya Jiji la Dar  na kusababisha kuvunjika kwa kifundo ‘enka’ cha mguu wa kulia hivyo kumsababishia kutembelea magongo baada ya hospitali kumuwekea ‘hogo’.

“Namshukuru Mungu kwanza kwa kunitoa salama katika ile ajali japokuwa sijapona vizuri,” alisema Madam Rita.
Mkurugenzi huyo aliendelea kueleza kuwa alipopata ajali hiyo alikimbizwa katika Hospitali ya Muhimbili kwenye Taasisi ya Mifupa ya Moi lakini hali ilipokuwa kuwa mbaya alihamia katika hospitali moja ya Kichina ambapo kwa sasa amepata nafuu" Alisema Madamu
.