Wednesday, November 6, 2013

MISS UNIVERSE TANZANIA ATAMBA MOSCOW

 
MISS Universe Tanzania, Betty Boniface Omara ametamba katika maonyesho ya mavazi kwa warembo 85 wanaowania taji la Miss Universe la mwaka huu mjini Moscow.

Katika mashindano hayo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Vegas Mall, vazi la Betty lililobuniwa na mbunifu anayekuja kwa kasi nchini, Mwanakombo Salim, lilipendwa na mashabiki wengi na anamatarajio makubwa kushinda taji hilo wakati wa fainali za mwaka huu zilizopangwa kufanyika Jumamosi.

Vazi hilo limechorwa na wasanii wa Tingatinga, Said Kambili na Mimus, michoro ambayo ni maarufu nchini iliyoasisiwa na msanii maarufu wa zamani, hayati Edward Tingatinga. Vazi hilo hilo mbali ya kudumisha utamaduni wa Tanzania, pia limechorwa michoro mbali mbali ya kuvitangaza vivutio vya kitalii.

Vazi hilo pia lina nakshi za mkeka na miba ya  mnyama maarufu ajulikanaye kwa jina la Nungunungu. Vilevile pia umetumika kama njia ya kumuonyesha ndege Tausi kama inavyoonekana rangi za mkeka kwenye mkia na kilemba kichwani mwake.

Lengo kuu la nguo na michoro hii ni kutangaza kazi za mikono na  utalii wa Tanzania na miongoni mwa michoro iliyoonyeshwa ni Duma, Tembo na Twiga vilevile imeonyesha ndege na mali asili zipatikanazo Tanzania kama vile Tausi, vipepeo, mimea na Mlima Kilimanjaro.

Mashindano ya Miss Universe Tanzania 2013 yamedhaminiwa na hifadhi ya Taifa Tanapa. 



 

Wednesday, October 16, 2013

ANDAA KUKU WAKUOKWA

Vipimo:

 

*Kuku mzima        1


Tangawizi   na thomu          1 kijiko cha supu

Mtindi                                   3 vijiko vya supu

Rojo la ukwaju                     2 Vijiko vya supu

Pilipili mbichi                      1 kijiko cha supu

Chumvi                             kiasi

Bizari ya jiyrah (cummin poda) 1 kijiko cha chai

Bizari ya dania (coriander poda.1 kijiko cha chai

Paprika                            1 kijiko cha chai

Kungu manga ya unga      1/2 kijiko cha chai

Hiliki                                    1/2 kijiko cha chai

Mdalasini                              1/2 kijiko cha chai

Siki au ndimu                       3 Vijiko vya supu
 
 
 
 
 * Ukipenda muache na ngozi bila ya kumchuna au mtoe ngozi.
 
 
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
 
 
1.  Changanya tangawizi na thomu, pilipili mbichi pamoja na vitu vyote vingine katika kibakuli.

2.  Mpasue kuku kidogo (slit) kila mahali kuweka njia ya kuweka huo mchanganyiko wa rojo la kuvumbika.

3.  Mtie hilo rojo kila sehemu na muacha avumbike (marinade) kwa muda wa masaa mengi katika friji.

4.  Paka mafuta kidogo katika treya umuweke kuku, kisha mchome katika oveni moto wa 450ยบ kwa muda wa dakika 45 hadi awive.

5.  Mtoe na umuweke katika sahani ya kupakulia ukipambia na saladi upendavyo.
 

Thursday, October 10, 2013

ROSE NDAUKA AKANA KUWA NA UJAUZITO WA MTARAJIWA WAKE.

Mwigizaji wa filamu Bongo Rose Ndauka akana kuwa na ujauzito huku Mtarajiwa wake Malick Bandawe akiwa akidai anafanya kila awezalo ili Rose aenjoy katika kipindi hiki cha ujauzito.

Na Mtarajiwa wake huyo ambaye naye pia ni Msanii wa Bongo fleva alipoulizwa kuhusu Ndoa alisema anasuburia  mpaka atakapojifungua mana kwa imani ya dini yake haruhusiwi kuoa mke ambaye ni mjamzito.

Zifuatazo ni baadhi ya picha wakiwa katika Hotel yenye hadhi ya Nyota tano.
 
 

MTOTO WA STELLA DAMASUS AKINGIA KWENYE UIGIZAJI.

Stella Damasus.
Binti wa mwigizaji maarufu wa Nigeria Stella Damasus ameingia kwenye fani ya mama yake.

Stella bila kutaja jina aliandika katika ukurasa wake wa Twitter
kuwa binti yake huyo atakuwa akionekana pia katika mtandao wa MixMatch, utakaokuwa ukirusha matukio ya kifamilia yatakayoandaliwa kama filamu kutoka New York marekani.

Stella Damasus ambaye pia ni muimbaji hajawahi kuzungumzia chochote kuhusu kuhusu ama kutokuwa tayari mtoto wake huyo kuingia katika fani yake ya uigizaji.

CHEZEEEAAA MADAM WEMA!!!

Hii imekuja baada ya Diamond ku-post katika account yake ya Instagram kua wako katika Zoezi la kushoot movie mpya iitwayo TEMPTATIONS yeye na Wema  huko China. Haya tusubiri tuone mana hata Penny tuliambiwa wanashut muvi mpyaaaaaaaaaa ikwa muviiiiiiii!!!!
Wema akiwa na Diamond katika moja ya mitaa huko Hong Kong China.
 

Wednesday, October 9, 2013

CHRISTINA MILIAN ASEMA PENZI LAKE KWA JAS PRICE NI LA MILELE

 

Mwanamuziki na mwigizaji Christina Milian amefunguka kuhusu penzi lake kwa Jas Price akiweka wazi kwamba ni la milele na hakuna wa kulivuruga.

Milian alisema mtu yeyote hawezi kuvuruga penzi lao kwa namna yeyote ile kwani ni uhusiano wa muda mrefu ambao wameweza kudumu kwa muda wa miaka mitatu.

"Jas ajanivisha pete lisha ya kuwa kwenye uhusiano naye kwa muda wa miaka mitatu, lakini naamini hiyo siyo ishara ya kunichoka na kuvunja uhusiano wetu"Alisema Milian.

KARAN JOHAR: HAKUNA KAMA KUCH KUCH HOTA HAI

MWIGIZAJI kutoka Bollywood India Karan Johar amekiri kuikubali sana filamu ya Kuch Kuch Hota Hai, kwa kusema ni filamu ya karne.

Akizungumza na mtandao wa India Express Johar alisema amewahi kutunga na kucheza filamu nyingi lakini hakuna ambayo inapita filamu hiyo kati ya zoote.


Johar alisema amewahi  kucheza na kuandaa ila filamu ya Kuch Kuch Hota Hai ndio filamu yake bora katika soko la filamu la Bollywood.

"kwangu Kuch Kuch Hota Hai ni filamu ya karne ni ya muda mrefu ila bado ndio filamu yangu bora katika soko la filamu la India mpaka leo"Alisema Johar