Thursday, September 26, 2013

MAMBO YA KUZINGATIA KABLA YA KUPAKA MAKE'UP

Vipodozi au Makeups ni urembo unaopendwa zaidi na wanawake wengi, dhamira yao ikiwa ni kubadili muonekano wao uliozoeleka ili wapendeze.

Mara nyingi watu wanapopaka makeups tofauti hujitokeza usoni kutokana na kipodozi hicho kufanya kazi ya kung'arisha na kupendezesha uso.

Unapofika wakati wa kupaka makeups,kwanza unapaswa kuchagua ni ipi itakufaa na kukupendeza. swali la kam kipi kitafaa zaidi kati ya poda au cream,hilo linabaki kwa mhusika kwa kuwa kila mmoja anapendekezo lake,kutokana namna anavyopata matokeo mazuri.


MAMBO YAKUZINGATIA KABLA YA KUPAKA MAKEUPS.

Kwanza jaribu kutafuta make ups inayoendana na ngozi yako na rangi ya mwili wako.

Watu wenye ngozi za mafuta wanashauriwa  kupaka makeup ya poda au unga unga kwani ya cream inaweza kuziba vitundu vya hewa katika ngozi ya uso.

Kwa walio na ngozi kavu wafahamu kuwa, make up ya cream haina uwezo wa kukaa kwa muda mrefu katika ngozi hivyo kama unahitaji kuwa nayo kwa muda unaozidi masaa nane unapaswa kupaka makeup ya poda iliyozoeleka na wengi.

Hakikisha unapaka makeup kwa kutumia brash zake maalum na si kitambaa au mikono.

No comments:

Post a Comment